-
Ezekieli 22:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Kama watu wanavyokusanya fedha na shaba na chuma na risasi na bati katika tanuru ili kuyapulizia moto madini hayo na kuyayeyusha, ndivyo nitakavyowakusanya ninyi kwa hasira yangu na kwa ghadhabu yangu, nami nitawapuliza na kuwayeyusha.+ 21 Nitawakusanya na kuwapuliza kwa moto wa ghadhabu yangu,+ nanyi mtayeyushwa ndani yake.+ 22 Kama fedha inavyoyeyushwa katika tanuru, ndivyo mtakavyoyeyushwa ndani yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimewamwagia ghadhabu yangu.’”
-