21 Nawe utasema moyoni mwako,
‘Ni baba gani aliyenizalia watoto hawa,
Kwa kuwa mimi ni mwanamke niliyefiwa na watoto, nami ni tasa,
Nami nilipelekwa uhamishoni na kufungwa?
Ni nani aliyewalea hawa?+
Tazameni! Nilibaki peke yangu,+
Sasa hawa wametoka wapi?’”+
22 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Tazameni! Nitayainulia mataifa mkono wangu,
Nami nitawainulia watu ishara yangu.+
Watawaleta wana wako wakiwa wamewabeba mikononi mwao
Na kuwabeba mabinti wako kwenye mabega yao.+