-
Luka 4:17-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Basi akapewa kitabu cha kukunjwa cha nabii Isaya, akakifungua na kupata mahali palipoandikwa: 18 “Roho ya Yehova* iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta ili niwatangazie maskini habari njema. Alinituma niwatangazie mateka uhuru na vipofu kuona tena, kuwaweka huru waliopondeka,+ 19 kuhubiri mwaka wa Yehova* unaokubalika.”+ 20 Ndipo akakikunja kitabu hicho na kumrudishia mtumishi, kisha akaketi; na wote katika sinagogi walikuwa wakimtazama kwa makini. 21 Akaanza kuwaambia: “Leo andiko hili ambalo mmetoka kusikia limetimia.”+
-
-
Matendo 26:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Nami nitakuokoa kutoka kwa watu hawa na kutoka kwa mataifa ambayo ninakutuma kwao+ 18 ili kuwafungua macho,+ kuwageuza watoke gizani+ waingie kwenye nuru+ na watoke kwenye mamlaka ya Shetani+ wamgeukie Mungu, ili wasamehewe dhambi zao+ na kupata urithi miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
-