-
Kumbukumbu la Torati 13:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “Ikiwa nabii au mtu anayebashiri kupitia ndoto atatokea miongoni mwenu na kuwapa ishara au dalili ya ajabu, 2 kisha ishara au dalili hiyo aliyowaambia itimie wakati anaposema, ‘Acheni tuifuate miungu mingine, miungu msiyoijua, na acheni tuiabudu,’ 3 hampaswi kusikiliza maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue ikiwa mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+
-