3 Nilisema: “Sikieni, tafadhali, enyi viongozi wa Yakobo
Nanyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+
Je, hampaswi kujua jambo lililo la haki?
2 Lakini mnachukia mema+ na kupenda maovu;+
Mnawachuna ngozi watu wangu na kuondoa nyama kutoka kwenye mifupa yao.+
3 Pia mnakula nyama ya watu wangu+
Na kuwachuna ngozi,
Mnapasua mifupa yao, na kuivunja vipandevipande,+
Kama kitu kinachopikwa ndani ya chungu, kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.