32 “‘Kwa hiyo Yehova anasema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru:+
“Hataingia katika jiji hili+
Wala hatapiga mshale humo
Wala kulikabili kwa ngao
Wala kujenga boma la kulizingira.+
33 Atarudi kupitia njia aliyotumia kuja;
Hataingia katika jiji hili,” asema Yehova.
34 “Nitalilinda jiji hili+ na kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+
Na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+