-
2 Wafalme 19:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Usiku huohuo malaika wa Yehova alienda na kuwaua wanaume 185,000 katika kambi ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, waliona maiti zote hizo.+ 36 Kwa hiyo Mfalme Senakeribu wa Ashuru akaondoka, akarudi Ninawi+ na kukaa huko.+ 37 Alipokuwa akiinama chini katika nyumba ya* Nisroki mungu wake, watoto wake mwenyewe wa kiume Adrameleki na Shareza walimuua kwa upanga+ na kutorokea nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwanawe akawa mfalme baada yake.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 32:21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Ndipo Yehova akamtuma malaika, na malaika huyo akamwangamiza kabisa kila shujaa hodari,+ kiongozi, na mkuu katika kambi ya mfalme wa Ashuru, hivi kwamba akarudi katika nchi yake akiwa ameaibika. Baadaye aliingia katika nyumba ya* mungu wake, na humo baadhi ya wanawe mwenyewe wakamuua kwa upanga.+
-