48 Sikieni hili, enyi watu wa nyumba ya Yakobo,
Ninyi mnaojiita kwa jina la Israeli+
Na ambao mmetoka katika maji ya Yuda,
Ninyi mnaoapa kwa jina la Yehova+
Na mnaomwitia Mungu wa Israeli,
Ingawa si katika kweli na uadilifu.+
2 Kwa maana wanajiita kwa jina la jiji takatifu+
Na kutafuta msaada wa Mungu wa Israeli,+
Ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.