-
Yeremia 52:31-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Kisha katika mwaka wa 37 tangu Mfalme Yehoyakini+ wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, katika mwezi wa 12, siku ya 25 ya mwezi huo, Mfalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka alioanza kutawala, alimwachilia huru Mfalme Yehoyakini wa Yuda na kumtoa gerezani.+ 32 Alizungumza naye kwa fadhili na kukikweza kiti chake cha ufalme juu zaidi kuliko viti vya wafalme wengine waliokuwa pamoja naye Babiloni. 33 Basi Yehoyakini akavua mavazi yake ya gerezani, na sikuzote za maisha yake alikuwa akila kwenye meza ya mfalme. 34 Naye alipewa chakula kwa ukawaida kutoka kwa mfalme wa Babiloni, siku baada ya siku, mpaka siku aliyokufa, siku zote za maisha yake.
-