-
Mathayo 2:16-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Herode alipoona ameshindwa akili na wale wanajimu, akakasirika sana, akaamuru wavulana wote huko Bethlehemu na wilaya zake zote wauawe, kuanzia umri wa miaka miwili kwenda chini, kulingana na wakati aliokuwa amehakikisha kwa uangalifu kutoka kwa wale wanajimu.+ 17 Ndipo yakatimia maneno haya yaliyosemwa kupitia nabii Yeremia: 18 “Sauti ilisikika kule Rama, kilio na kuomboleza kwingi. Raheli+ akiwalilia watoto wake, naye hakutaka kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”+
-