-
Ezekieli 29:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninampa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atabeba utajiri wake na kuchukua nyara kwa wingi na kuipora; na vitu hivyo vitakuwa malipo ya jeshi lake.’
20 “‘Kama malipo ya kazi kubwa aliyofanya ya kushambulia Tiro, nitampa nchi ya Misri kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
-