6 Nikasema: “Ee Mungu wangu, ninaona aibu na haya kuuinua uso wangu kwako, Ee Mungu wangu, kwa sababu makosa yetu yameongezeka juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imerundamana mpaka mbinguni.+
7 Ee Yehova, uadilifu ni wako, lakini aibu ni yetu kama ilivyo leo, sisi watu wa Yuda, wakaaji wa Yerusalemu, na Waisraeli wote, wale walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ambazo uliwatawanya kwa sababu hawakutenda kwa uaminifu kukuelekea.+