-
Mwanzo 32:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Mwishowe Yakobo akabaki peke yake. Kisha mwanamume fulani akaanza kupigana naye mweleka mpaka kulipopambazuka.+ 25 Mwanamume huyo alipoona kwamba hajamshinda Yakobo, akamgusa kiungio cha nyonga; na kiungio cha nyonga ya Yakobo kikateguka alipokuwa akipigana naye mweleka.+ 26 Kisha mwanamume huyo akasema: “Niache niende, kwa maana kunapambazuka.” Yakobo akamwambia: “Sitakuacha uende mpaka unibariki.”+
-