Kumbukumbu la Torati 33:2 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 2 Alisema hivi: “Yehova—alikuja kutoka Sinai,+Naye akawaangazia kutoka Seiri. Aliangaza kwa utukufu kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+Naye alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+Na mashujaa wake kwenye mkono wake wa kuume.+ Waamuzi 5:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 Yehova, ulipotoka Seiri,+Ulipopiga mwendo kutoka eneo la Edomu,Dunia ilitikisika, na mbingu zikamwaga maji,Naam, mawingu yakamwaga maji. Zaburi 68:7, 8 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 7 Ee Mungu, ulipowaongoza* watu wako,+Ulipopiga mwendo jangwani, (Sela) 8 Dunia ilitetemeka;+Mbingu zilinyesha* mvua kwa sababu ya Mungu;Huu Mlima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+
2 Alisema hivi: “Yehova—alikuja kutoka Sinai,+Naye akawaangazia kutoka Seiri. Aliangaza kwa utukufu kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+Naye alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+Na mashujaa wake kwenye mkono wake wa kuume.+
4 Yehova, ulipotoka Seiri,+Ulipopiga mwendo kutoka eneo la Edomu,Dunia ilitikisika, na mbingu zikamwaga maji,Naam, mawingu yakamwaga maji.
7 Ee Mungu, ulipowaongoza* watu wako,+Ulipopiga mwendo jangwani, (Sela) 8 Dunia ilitetemeka;+Mbingu zilinyesha* mvua kwa sababu ya Mungu;Huu Mlima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+