-
Amosi 1:13-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu ya maasi matatu ya Waamoni,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,
Kwa sababu waliwapasua tumbo wanawake wenye mimba wa Gileadi ili wapanue eneo lao wenyewe.+
14 Basi nitaushushia moto ukuta wa Raba,+
Nao utateketeza kabisa ngome zake zenye minara,
Kwa kelele za vita katika siku ya mapigano,
Kwa tufani katika siku ya kimbunga.
15 Na mfalme wao atapelekwa uhamishoni pamoja na wakuu wake,”+ asema Yehova.’
-