-
Ezekieli 22:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Ndani yake manabii wake wamepanga njama,+ kama simba anayenguruma akirarua mawindo.+ Wanawanyafua watu. Wanachukua hazina na vitu vyenye thamani. Wamewafanya wengi kuwa wajane ndani yake. 26 Makuhani wake wamevunja sheria yangu,+ nao wanaendelea kupatia unajisi mahali pangu patakatifu.+ Hawatofautishi kati ya kitu kitakatifu na cha kawaida,+ hawawajulishi watu kisicho safi na kilicho safi,+ na wanakataa kushika sabato zangu, nami nimechafuliwa kati yao.
-