6 “Siku hiyo,” asema Yehova,
“Nitamkusanya yule aliyekuwa akichechemea,
Na kumkusanya pamoja yule aliyetawanyika,+
Pamoja na wale niliowatesa.
7 Nitamfanya yule aliyekuwa akichechemea abaki,+
Na yule aliyepelekwa mbali kuwa taifa lenye nguvu;+
Na Yehova atawatawala akiwa mfalme katika Mlima Sayuni,
Kuanzia sasa mpaka milele.