16 “Yehova, Mungu anayewapa watu wote uhai,* naomba umchague mwanamume atakayewasimamia watu hawa 17 ili awatangulie na kuwaongoza katika mambo yote, ili watu hawa wa Yehova wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
17 Basi Mikaya akasema: “Ninawaona Waisraeli wote wakiwa wametawanyika milimani,+ kama kondoo wasio na mchungaji. Yehova akasema: ‘Hawa hawana bwana. Acha kila mmoja wao arudi kwa amani nyumbani kwake.’”
34 Basi, aliposhuka, akaona umati mkubwa, akawasikitikia,+ kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.+ Naye akaanza kuwafundisha mambo mengi.+