-
Marko 7:18-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Basi akawaambia: “Je, ninyi pia hamwelewi kama wao? Je, hamjui kwamba mtu hawezi kuchafuliwa na kitu kinachoingia ndani yake, 19 kwa kuwa hakiingii moyoni mwake bali huingia tumboni, kisha hutoka na kuingia chooni?” Kwa hiyo akatangaza vyakula vyote kuwa safi. 20 Tena akasema: “Kile kinachotoka ndani ya mtu ndicho humchafua.+ 21 Kwa maana kutoka ndani, moyoni mwa watu,+ hutoka mawazo mabaya: uasherati,* wizi, mauaji, 22 uzinzi, pupa, uovu, udanganyifu, mwenendo mpotovu,* jicho lenye wivu, makufuru, majivuno, na ukosefu wa akili. 23 Mambo hayo yote maovu hutoka ndani, nayo humchafua mtu.”
-