-
Mathayo 6:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 “Iweni waangalifu msionyeshe uadilifu wenu mbele ya watu ili wawaone;+ la sivyo hamtapata thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni. 2 Basi unapotoa zawadi za rehema,* usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki katika masinagogi na barabarani, ili wasifiwe na watu. Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili.
-