-
Luka 21:21-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Ndipo wale walio Yudea waanze kukimbilia milimani,+ na wale walio Yerusalemu waondoke, nao wale walio mashambani wasiingie ndani yake, 22 kwa sababu hizi ni siku za kutekeleza haki,* ili mambo yote yaliyoandikwa yatimizwe. 23 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto katika siku hizo!+ Kwa maana kutakuwa na mateso mengi katika nchi na ghadhabu dhidi ya watu hawa.
-