-
Marko 14:55-59Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
55 Sasa wakuu wa makuhani na Sanhedrini yote walikuwa wakitafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wamuue, lakini hawakupata.+ 56 Kwa kweli, wengi walikuwa wakitoa ushahidi wa uwongo kumhusu,+ lakini ushahidi wao haukupatana. 57 Pia, wengine walikuwa wakisimama na kutoa ushahidi wa uwongo kumhusu, wakisema: 58 “Tulimsikia akisema, ‘Nitaliangusha chini hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine ambalo halijajengwa kwa mikono.’”+ 59 Lakini hata kwa misingi hiyo, ushahidi wao haukupatana.
-