-
Marko 15:16-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Sasa wanajeshi wakampeleka kwenye ua, katika makao ya gavana, nao wakakusanya kikosi chote cha wanajeshi.+ 17 Wakamvika Yesu vazi la zambarau, wakasokota taji la miiba na kumvisha; 18 nao wakaanza kumwambia kwa sauti kubwa: “Salamu,* ewe Mfalme wa Wayahudi!”+ 19 Pia, walikuwa wakimpiga kichwani kwa utete na kumtemea mate, nao wakapiga magoti na kumsujudia.* 20 Mwishowe, baada ya kumdhihaki, wakamvua lile vazi la zambarau na kumvisha mavazi yake ya nje. Kisha wakampeleka ili kumtundika mtini.+
-