-
Luka 22:10-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Akawaambia: “Tazameni! Mtakapoingia jijini, mtakutana na mwanamume akiwa amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mwingie katika nyumba atakayoingia.+ 11 Mwambieni mwenye nyumba hiyo, ‘Mwalimu anasema: “Kiko wapi chumba cha wageni ambamo ninaweza kula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?”’ 12 Mtu huyo atawaonyesha chumba kikubwa cha juu chenye vifaa. Tayarisheni humo.” 13 Basi wakaenda na kupata kama alivyokuwa amewaambia, nao wakaandaa Pasaka.
-