-
Mathayo 13:31, 32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Akawatolea mfano mwingine akisema: “Ufalme wa mbinguni ni kama mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.+ 32 Kwa kweli, mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua huwa kubwa kuliko mimea yote ya mboga na huwa mti, hivi kwamba ndege wa angani huja na kupata makao katika matawi yake.”
-
-
Marko 4:30-32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Akaendelea kusema: “Tutaufananisha Ufalme wa Mungu na nini, au tutatumia mfano gani kuufafanua? 31 Ni kama mbegu ya haradali, ambayo ilipopandwa katika udongo ilikuwa ndogo kuliko mbegu zote duniani.+ 32 Lakini baada ya kupandwa, humea na kuwa kubwa kuliko mboga nyingine zote na kutokeza matawi makubwa, hivi kwamba ndege wa angani hupata makao chini ya kivuli chake.”
-