-
Mathayo 27:5-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Basi akavitupa vile vipande vya fedha hekaluni. Kisha akaenda zake akajinyonga.+ 6 Lakini wakuu wa makuhani wakachukua pesa hizo wakasema: “Si halali kuziweka katika hazina takatifu, kwa sababu ni bei ya damu.” 7 Baada ya kushauriana, wakatumia pesa hizo kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni. 8 Kwa hiyo, shamba hilo limeitwa Shamba la Damu+ hadi leo hii.
-