-
Matendo 11:5-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 “Nilipokuwa nikisali katika jiji la Yopa, niliona maono katika njozi, kitu fulani* kikishuka kama shuka kubwa la kitani, kikiteremshwa kutoka mbinguni kwa ncha zake nne, nacho kikaja moja kwa moja mpaka mahali nilipokuwa.+ 6 Nilipotazama kwa makini ndani yake, nikaona wanyama wa dunia wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, viumbe wanaotambaa, na ndege wa angani. 7 Pia nikasikia sauti ikiniambia: ‘Petro, simama, chinja ule!’ 8 Lakini nikasema, ‘Hapana Bwana, kwa sababu kitu chochote najisi au kisicho safi hakijawahi kamwe kuingia kinywani mwangu.’ 9 Mara ya pili, ile sauti kutoka mbinguni ikajibu: ‘Wewe acha kuviita najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.’ 10 Hilo likatokea mara ya tatu, na kila kitu kikavutwa juu kurudi mbinguni.
-