-
Matendo 10:30-33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Ndipo Kornelio akasema: “Siku nne zilizopita wakati kama huu, nilikuwa nikisali katika nyumba yangu saa tisa;* wakati huohuo mwanamume aliyevaa mavazi yanayong’aa akasimama mbele yangu 31 na kusema: ‘Kornelio, sala yako imesikiwa na kukubaliwa, naye Mungu amezikumbuka zawadi zako za rehema. 32 Kwa hiyo, tuma watu waende Yopa wakamwite Simoni anayeitwa Petro. Mtu huyu ni mgeni katika nyumba ya Simoni, mtengenezaji wa ngozi, kando ya bahari.’+ 33 Mara moja nikawatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kuja hapa. Basi sote tupo mbele za Mungu ili kuyasikia mambo yote ambayo Yehova* amekuamuru useme.”
-