24 Kwa maana mtu fulani aliyeitwa Demetrio, fundi wa fedha aliyetengeneza vihekalu vya fedha vya Artemi, aliwaletea mafundi faida kubwa.+ 25 Akawakusanya pamoja na wengine waliofanya kazi kama hiyo na kuwaambia: “Wanaume, mnajua vema kwamba tunapata mafanikio yetu kutokana na biashara hii.