12 Wapendwa, msishangazwe na majaribu makali yanayowapata,+ kana kwamba mnapatwa na jambo geni. 13 Badala yake, endeleeni kushangilia+ kwa kadiri ambayo ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo,+ ili mshangilie na kuwa na shangwe sana pia wakati wa ufunuo wa utukufu wake.+