19 bali ilikuwa kwa damu yenye thamani,+ kama ile ya mwanakondoo asiye na dosari+ na asiye na doa, ile ya Kristo.+20 Ni kweli, yeye alijulikana mapema kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu,+ lakini alifunuliwa mwishoni mwa nyakati kwa ajili yenu.+
12 nao walikuwa wakisema kwa sauti kubwa: “Mwanakondoo aliyechinjwa+ anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”+