6 Basi tukikabili majaribu,* ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; na tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu inayotenda ili kuwasaidia mvumilie mateso yaleyale ambayo sisi pia tunateseka.
24 Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami ninakabili dhiki za Kristo ambazo bado hazimo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake,+ ambao ni kutaniko.+
8 Basi, kwa maana tulikuwa na upendo mwororo kwenu, tulijitahidi* kuwapa habari njema ya Mungu na hata uhai wetu* wenyewe,+ kwa sababu tuliwapenda sana.+
17 Watiini wale wanaoongoza kati yenu+ na mnyenyekee,+ kwa maana wanaendelea kuwalinda ninyi* kama wale watakaotoa hesabu,+ ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa huzuni, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.