21 Kwa maana kutoka ndani, moyoni mwa watu,+ hutoka mawazo mabaya: uasherati,* wizi, mauaji, 22 uzinzi, pupa, uovu, udanganyifu, mwenendo mpotovu,* jicho lenye wivu, makufuru, majivuno, na ukosefu wa akili.
4 Kwa maana watu fulani wameingia kisiri kati yenu ambao Maandiko yalisema tangu zamani kwamba wanastahili hukumu; watu hao hawamwogopi Mungu, wanazitumia fadhili zisizostahiliwa za Mungu wetu kuwa kisingizio cha mwenendo mpotovu*+ wakimkana mmiliki* wetu pekee na Bwana wetu, Yesu Kristo.+