3 Ndipo Sauli akaanza kulishambulia kutaniko. Alikuwa akivamia nyumba moja baada ya nyingine, akiwakokota nje wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.+
9Lakini Sauli aliendelea kuwatisha wanafunzi wa Bwana akitaka kuwaua,+ basi akamwendea kuhani mkuu 2 na kumwomba barua za kwenda kwenye masinagogi huko Damasko, ili awakamate wanaume na wanawake walioifuata Ile Njia,+ na kuwaleta Yerusalemu wakiwa wamefungwa.
13 Bila shaka, mlisikia kuhusu mwenendo wangu wa zamani katika dini ya Kiyahudi,+ kwamba niliendelea kulitesa sana* kutaniko la Mungu na kuliangamiza;+
5 nilitahiriwa siku ya nane,+ mimi ni wa taifa la Israeli, wa kabila la Benjamini, Mwebrania aliyezaliwa kwa Waebrania;+ kuhusu sheria, Farisayo;+6 kuhusu bidii, nililitesa kutaniko;+ kuhusu uadilifu unaotegemea sheria, mtu ambaye hakuwa na hatia.