-
Mathayo 5:34-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 Hata hivyo, ninawaambia: Msiape kamwe+ kwa mbingu kwa sababu ni kiti cha ufalme cha Mungu; 35 wala kwa dunia kwa sababu ni mahali pake pa kuwekea miguu;+ wala kwa Yerusalemu kwa sababu ni jiji la Mfalme mkuu.+ 36 Usiape kwa kichwa chako kwa sababu huwezi kugeuza unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Acheni ‘Ndiyo’ yenu imaanishe ndiyo, na ‘Siyo’ yenu, siyo,+ kwa maana linalozidi hayo linatoka kwa yule mwovu.+
-