5 Sasa ikiwa mtaitii kabisa sauti yangu na kushika agano langu, hakika mtakuwa mali yangu ya pekee* kati ya mataifa yote,+ kwa maana dunia yote ni mali yangu.+6 Mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’+ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”
6 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu, na Yehova Mungu wenu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali yake ya pekee,* kutoka kati ya mataifa yote yaliyo duniani.+
15 Lakini Yehova aliwakaribia na kudhihirisha upendo wake kwa mababu zenu tu, naye amewachagua ninyi, wazao wao,+ kutoka kati ya mataifa yote, kama mlivyo leo.
17 “Nao watakuwa wangu,”+ asema Yehova wa majeshi, “siku nitakayotokeza mali ya pekee.*+ Nitawahurumia, kama mwanamume anavyomhurumia mwana wake anayemtumikia.+