-
Ufunuo 19:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Baada ya hayo nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati mkubwa mbinguni. Wakasema: “Msifuni Yah!*+ Wokovu na utukufu na nguvu ni za Mungu wetu, 2 kwa sababu hukumu zake ni za kweli na za uadilifu.+ Kwa maana ametekeleza hukumu juu ya yule kahaba mkubwa aliyeipotosha dunia kwa uasherati* wake, naye amelipiza kisasi damu ya watumwa wake iliyo mkononi mwake.”*+
-