Ukurasa wa Pili
Kuvuta au kutovuta sigareti, hilo ndilo swali. Kwa kawaida mtu hukabili swali hilo akiwa kijana tineja. Hakuna sharti lenye kuhusika. Ni uamuzi wa hiari ya mtu. Lakini kulingana na wenye mamlaka ya tiba, huo ni uamuzi ambao ungeweza kuwa na matokeo mazito katika maisha yako. Ungeweza hata kuamua utakufa wakati gani na jinsi gani.
Kwa hiyo, maswali ya maana yatokezwa: Je! ni tabia njema kutangaza bidhaa za tumbako? Je! laweza kutetewa kuwa jambo lenye haki ya kiadili kwa yale yaitwayo eti mataifa ya Kikristo kusafirisha bidhaa zayo za tumbako, huku yakizipakua juu ya mataifa mengine? Je! wauzaji wa sigareti wanauza ugonjwa na kifo? Na kwa kuwa watu ndio huchagua kuvuta sigareti, je! kuna ubaya wowote?