‘Maagizo ya Msingi ya Adili’
Msichana mmoja wa miaka 14 kutoka Naijeria, Afrika Magharibi, anashukuru kwa kupokea maagizo hayo kutoka kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Yeye anaandika hivi:
“Kitabu hiki ni kitu cha ufundi kilicho kizuri sana na chenye kupendeza ambacho kinachosaidia sana na chenye ukweli. Bila shaka kitakuwa msaada mkubwa kwa yeyote mwenye mbetuko wa kuongozwa ifaavyo kupita kasoro nyingi zenye dhambi maishani.
“Nimekifikisha kitabu hiki kwa wana-shule wenzangu na majirani. Kila mtu anayekisoma anasifu vielezi vyenu bora sana ‘vyenye kusitawisha maarifa’ na habari zilizozungumzwa ndani ya kitabu hiki. Sisi tuna maoni kwamba kweli zilizoonyeshwa ndani ya kitabu hiki hazitatia tu maarifa au kutia hekima na kanuni za mwenendo zilizo za lazima, bali pia zaweza kuandaa miongozo chanya kwa vijana na watu wazima wanaotamani kuonea shangwe amani ya kweli ya akili na afya, na ambao wangezoea kujidhibiti na kuonyesha wana nguvu kuelekea yaliyo sahihi. . . .
“Juu ya yote, kitabu hiki kina mengi mno na kimejaa pomoni maagizo ya msingi ya adili za kingono yasiyoweza kupatikana kutoka kwa wengi wa wazazi au walimu . . . Natamani sana kitabu hiki kitumiwe kwenye mashule kwa ajili ya masomo ya darasani ya kila siku, ili kutokeza mtindo wa maisha wenye amani zaidi, wenye kupendeka, wenye kuzaa matunda na wenye maana.”
Kupata Faida Zote za Ujana Wako kinajibu maswali kama vile, Ni kwa nini vijana wanapaswa kujifunza shuleni? Wawaoneje wazazi wao? Je! wajifunze wawe na mahusiano ya kingono kabla ya ndoa? Je! wanywe vileo? Pokea nakala moja kwa Kshs 20/- tu (Tshs 150/-; RWF 100/-) kwa kujaza na kupeleka kuponi hii.
Tafadhali mnipelekee kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192, Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Nawapelekea Kshs. 20/- (Tshs. 150/-; RWF 100/-).