“Gazeti la Upendezi wa Ujumla Lililo Bora Zaidi Ulimwenguni”
HIVYO Ndivyo barua moja mwaka jana iliyopelekewa ofisi ya tawi ya ya Mashahidi wa Yehova ya Naijeria ilivyolieleza Amkeni! Mwandikaji alifafanua hivi:
“Mimi nafanya kazi na gazeti Eko, kichapo cha jiji cha Newswatch, gazeti la kimataifa la Naijeria lisomwalo zaidi ya mengine nchini. Nimekuwa mwandikishaji wa Amkeni! tangu 1985, ingawa mimi si Shahidi. Juzi tulipokuwa tukitokeza chapa ambayo ingefuata ya Eko, niliacha mezani Amkeni! nililokuwa nikisoma [Oktoba 8, 1991] ili nishughulikie kazi fulani dogo.
“Mmojapo wafanyakazi wenzangu alilichukua alitupie jicho kwa haraka, lakini akatumia wakati akisoma mfululizo mzima wa makala juu ya talaka. Mtu mwingine alipata gazeti hilo, na mwingine tena, na mwingine tena. Mmoja wao, Mkristo mwenye kuzoea Othodoksi, aliniambia kwamba alizoea kupuuza Amkeni! naye hakufikiri kamwe mngeweza kuandika ‘makala zenye kupendeza, zenye kuelimisha kwa njia yenye kushangaza jinsi hiyo,’ naye aliniuliza mara hiyo jinsi anavyoweza kuliandikisha. Mwingine aliniomba nimpe magazeti yangu kila wakati niyapokeapo.
“Kwelikweli, mimi sina tamaa ya kuwa Shahidi, hata hivyo sijapata kusikitikia uamuzi wangu wa kuandikisha Amkeni! Asanteni, na pongezi kwa gazeti la upendezi wa ujumla lililo bora zaidi ulimwenguni.”
Mashahidi wa Yehova ni tengenezo la kimataifa la Wanafunzi wa Biblia zaidi ya milioni nne ambao wamejitoa kusaidia watu wajifunze zaidi juu ya makusudi ya Mungu.
Ikiwa ungependa habari zaidi kuhusu Mashahidi wa Yehova na imani zao, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.