“Hiki Chaonekana Kuwa Kitabu Ambacho Ningependa Kusoma Mwenyewe”
JESSICA, mwanafunzi wa miaka 16 kwenye shule ya upili ya Jiji la New York, aliandikia Amkeni!: “Nina mwalimu wa historia ambaye hakuna mtu, hata mmoja, ampendaye. Alipatia kikundi cha darasa mgawo juu ya ‘Dini Zilizo Kuu.’ Kikundi changu kilipata Uislamu. Sikuwa na wasiwasi kwa kuwa nilijua ningepata habari ya kutosha katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Nilitayarisha ripoti nzuri zaidi kadiri nilivyoweza.
“Siku ilifika ambayo kikundi chetu kilitoa ripoti yetu kwa kuisoma. Mwalimu huyo alikuwa akikatiza na kuwapigia kelele wanafunzi, kwa hiyo nilipata wasiwasi kidogo. Ilipofika zamu yangu, niliambia darasa kuhusu mambo ya pekee ya Uislamu. Nilipitisha kitabu Kutafuta Mungu, nikiwaagiza wanafunzi watazame picha kwenye kurasa 286 na 289. Mwalimu alipopitia kitabu hicho, alinikatiza na kusema, ‘Kunradhi, je, hiki ni kitabu chako? Je! nibaki nacho kidogo? Nilijibu, ‘Ninaweza kukuletea nakala yako ukipenda.’ Uso wake ukaonyesha furaha, na akasema: ‘Hilo ni jambo zuri sana. Hiki chaonekana kuwa kitabu ambacho ningependa kusoma mwenyewe.’ Moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu sana kwa msisimko na mshangao, niliguguna tu katika sehemu iliyobaki ya ripoti yangu.
“Alinipatia mojawapo maksi za juu sana darasani (95) kwa ripoti hiyo. Ninamshukuru Yehova Mungu na ninyi ndugu kwa kutupatia kifaa chenye thamani Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.”
Ikiwa ungependa kupata habari zaidi kuhusu jambo lolote lililotajwa katika gazeti hili au unatamani kupata funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali jihisi huru kuandikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya.
[Picha katika ukurasa wa 32]
JITIHADA YA AINABINADAMU YA KUTAFUTA MUNGU