Walimu Watoa Fikira kwa Uumbaji
Shule moja katika Berlin, Ujerumani, ilionyesha picha kwenye ukuta mkubwa iliyoonyesha jinsi viumbe walio kama nyani walivyogeuka kuwa mwanadamu wa kisasa. Wanafunzi walipokuja shuleni siku moja, walipata kwamba picha hiyo ilikuwa imefutwa kwa rangi nyeupe. Ni nini kilichokuwa kimetukia?
Mwanafunzi mwenye miaka 16 aitwaye Natalie, mmoja wa Mashahidi wa Yehova, alimuuliza mwalimu wa biolojia sababu ya picha hiyo kuondolewa. Mwalimu alieleza kwamba mwanafunzi mmoja alikuwa amempa nakala ya kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Kitabu hicho kilimvutia sana hivi kwamba alikionyesha kwa walimu wengine wa biolojia. Wao pia walivutiwa nacho.
Hivyo, walimu hao walifanya uamuzi wa kufuta mchoro ule, kama walivyosema, ‘ili kuzuia kuchochea vibaya akili za wanafunzi kimbele.’ Kwa hiyo badala ya kufunza wanafunzi nadharia ya mageuzi tu, walimu hao walipanga pia kufundisha juu ya uumbaji, wakitumia habari katika kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?
Kichapo hicho chenye kuvutia hutangazwa na Mashahidi wa Yehova, tengenezo la kimataifa la wanafunzi wa Biblia zaidi ya milioni nne ambao wamejitoa kusaidia watu wajifunze zaidi kuhusu makusudi ya Mungu. Ikiwa ungependa kupata habari zaidi au funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Life—How did it get here? By evolution or by creation?