Msaada kwa Watu Wenye Uhitaji
Msaada ndio jambo ambalo watu wenye nia njema hutaka kuandaa. Lakini msaada wa aina gani? Na waweza kuandaliwaje? Mtu mmoja mwenye fadhili aliandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Uholanzi mwezi Oktoba uliopita na akaeleza jinsi ambavyo angependa kuandaa msaada.
“Jumamosi iliyopita,” akaeleza, “Nilipewa trakti ndogo yenye kichwa Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Nafikiri hiyo ni trakti nzuri na yenye kueleweka iliyo na ujumbe mzuri. Inaonekana kwangu kwamba yafaa watu wenye matatizo makubwa, watu wanaohitaji msaada kwelikweli, watu ambao wangefurahi kusoma trakti kama hiyo.
“Karibu na shule yangu, Laurenskerkplein katika Rotterdam, siku zote watu kadhaa wanaozurura, walevi, na wenye kutumia dawa za kulevya wanaoketi tu. Ningependa kupokea hesabu fulani za trakti kutoka kwenu, ambazo naweza kuwatolea. Sitafanya hivyo kwa njia ya kuwalazimisha kamwe. Wazo langu ni kwamba niwape kitu ambacho kinanipendeza ninapopita.
“Natumaini mtanisaidia kwa njia hiyo. Nawatakia mafanikio sana katika kazi yenu!”
Mashahidi wa Yehova wamejitoa kusaidia watu wajifunze zaidi juu ya makusudi ya Mungu. Kama ungependa nakala ya trakti iliyotajwa hapo juu au watamani funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., BOX 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani