‘Inafariji Kujua Kwamba Mtu Fulani Ajali’
Watu fulani huonekana kuwa wazima, lakini kumbe wanahisi vibaya sana. Ni nini kinachoweza kusaidia? Hangaiko na uelewevu ni wa maana. Mwaka jana mtu kama huyo aliandikia Watch Tower Society katika Brooklyn, New York:
“Nimetoka tu kusoma trakti Faraja kwa Walioshuka Moyo. Mimi hupatwa na mshuko wa moyo wa mara kwa mara unaoletwa na kutosawazika kwa kikemia. Trakti hiyo inafariji sana.
“Inafariji kujua kwamba kuna tumaini kuhusu mshuko wa moyo na kwamba kuna njia za kukabiliana nao. Pia inafariji kujua kwamba mtu fulani anajali na kuwaelewa watu kama mimi wanaougua mshuko wa moyo.”
Maneno ya trakti hiyo yamejaa maana. Ikiwa ungependa nakala yayo au ungependa kupata habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Faraja kwa Walioshuka Moyo