Kilimfanya Asali
Karen, ambaye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika Jimbo la New York, alisema kwamba alimpelekea mama yake kitabu Kumsikiliza Mwalimu Mkuu. “Nilimpa mama kitabu hicho,” Karen akaandika, “ili mpwa wangu wa kike mwenye umri wa miaka tisa, Jamie, akisome wakati wa usiku.” Karen alieleza hivi: “Nilimwandikia Jamie barua na nikasema kwamba apaswa akisome kitabu hicho kila usiku katika nyumba ya nyanya, na angekuwa na mawazo mazuri kabla ya kulala.”
Mama ya Karen, ambaye si mmoja wa Mashahidi wa Yehova, baadaye aliambia Karen kwamba Jamie alienda kitandani na kuanza kusoma kitabu hicho. Asubuhi iliyofuata alisema Jamie alisali kwa ajili ya ndugu yake mchanga (ambaye angepasuliwa) kabla ya yeye kwenda kulala. Mama ya Karen alivutiwa sana na jambo hilo kwa sababu hakufikiria kwamba Jamie alikuwa amepata kusali wakati mwingine wowote.
Karen aliandika: “Ni kitabu chenye nguvu sana ikiwa kinaweza kufanya mtoto mwenye umri wa miaka tisa kusali baada ya kusoma sehemu ndogo tu yacho. Jambo hilo lilinifanya nithamini hata zaidi uwezo wa fasihi hiyo. Nafikiri kilivutia hata mama yangu kwa sababu alisema aliona kwamba kitabu hicho chauliza maswali mengi na kwa wazi chafundisha maadili na si hadithi tu.”
Ikiwa ungependa kupokea nakala ya Kumsikiliza Mwalimu Mkuu au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.