“Uandikaji Ni Mzuri Kabisa”
Barua ya uthamini iliijia Watch Tower Society kutoka kwa msomaji mmoja wa kike katika California, Marekani, ambamo alitaarifu hivi:
“Lile Amkeni! juu ya ‘Upweke—Unaloweza Kufanya Nao’ (Septemba 22, 1993) lanishurutisha kuchukua kalamu yangu niwaambie nimekuwa nikiyafurahia sana magazeti hivi majuzi. Uandikaji ni mzuri kabisa, na zile makala juu ya upweke ziliandikwa vema sana na zilikuwa za kishairi. Pia, niliuthamini usema-kweli wa makala hizo katika kuweka daraka la upweke kwa yule mtu mpweke mwenyewe. Kwa kweli makala hizo zaonyesha upendo wa kina kirefu wa Yehova na hangaikio lake la kuwajali watu wake.”
Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hugawanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Gazeti hilo lililotajwa kwanza, ambalo hutokeza mazungumzo yenye msingi wa Biblia juu ya masuala makubwa, huchapishwa kwa lugha 115, likiwa na uchapaji wa wastani wa nakala zaidi ya milioni 16 kila toleo. Gazeti lile la pili kutajwa, ambalo hutoa habari za kielimu juu ya mambo ya namna mbalimbali, hupatikana katika lugha 73 nalo lina uchapaji wa wastani wa nakala karibu milioni 13.
Ikiwa wewe ungependa kupokea matoleo ya sampuli za magazeti haya, tafadhali pashana habari na Mashahidi wa Yehova kwenye Jumba la Ufalme katika eneo lako, au uandikie anwani iliyo karibu zaidi na wewe iliyoorodheshwa katika ukurasa 5.