Majarida Yatimizayo Mahitaji ya Leo
Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—nakala zaidi ya milioni 58 huchapwa kila mwezi katika lugha zaidi ya mia moja—yamekuwa yakifanya hivyo hasa. Msomaji mwenye uthamini aliandika hivi:
“Asanteni sana kwa kuchapisha makala zishughulikiazo matatizo halisi yanayokabili wengi.” Pia alitaarifu hivi:
“Mwisho wa ulimwengu huu ukaribiapo, watu wahitaji hisiamwenzi, kueleweka, na ufahamu wenye kina kuwasaidia wakabili matatizo yao. Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanazidi kueleza sababu kwa nini nyakati fulani watu hushindwa kukabili . . .
“Walio wengi wataka kufanya yaliyo sawa, lakini mara nyingi wao hupambana na mivurugiko, hatia, hisiamoyo zisizofaa, hofu, kutojistahi sana, mazoea ya kufikiri kubaya, na hisia ya kwamba wako hoi kujisaidia. Makala zenu zinasaidia wengi kuanza tena kudhibiti maisha zao na hisiamoyo. . . .
“Nataka kuwashukuru hasa kwa Amkeni! la Januari 22, 1994 juu ya ‘Kuwasiliana Katika Ndoa.’ Badala ya kutoa mawazo ya kikawaida tu juu ya umaana wa kuwasiliana, nyinyi mwaeleza kindani sababu kwa nini wanaume na wanawake hushindwa kuelewana. Kwa kuwasaidia watu wawaelewe wenzi wao wa ndoa, mmesaidia sana wanadamu na mpango wa ndoa uliotoka kwa Mungu.”
Ikiwa ungependa kupelekewa nakala ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, tafadhali andikia I.B.S.A. Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa ukurasa wa 5