Vijana Waonyesha Uthamini
VIJANA waliopigwa picha hapa wote ni wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nigeria. Katika barua moja kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Nigeria, wao waliandika hivi: “Tungependa kuwashukuru kwa ufikirio ambao mmetuonyesha sisi vijana kwa kuchapisha kile kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.
“Kichapo hiki kimetusaidia kukinza misongo ya ulimwengu na kukanusha mafundisho yasiyo ya Kimaandiko. Chazungumzia kwa mapana mahangaikio mengi ya vijana, na mashauri yacho sikuzote huwa na msingi wa Biblia. Ile sehemu izungumziayo msongo wa marika imetusaidia hasa kuielewa hekima ya Biblia katika shauri layo la kutembea pamoja na wenye hekima na kuepuka ushirika pamoja na wapumbavu. Wanafunzi wale wengine katika shule yetu hustaajabia jinsi sisi huchukuliana katika upendo na jinsi tujitahidivyo kuushika umoja wa roho katika kile kifungo cha amani chenye kuungamanisha.
“Huku tukijitahidi nyakati zote kudumisha mwenendo mzuri miongoni mwa wanafunzi katika shule yetu, kwa bidii sisi hupigia mbiu lile tumaini la Ufalme kwa wanafunzi wote watakao kutusikiliza, bila kujali wale ambao huenda wakajaribu kutuvuta kwa njia mbaya.”
Barua hiyo ilitiwa sahihi, “Kutoka kwa vijana walio Mashahidi wa Yehova, Shule ya Sekondari ya All Saints, Aba, Jimbo la Abia, Nigeria.”
Ikiwa wewe ungependa kupokea nakala ya Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi au ungependa kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A. Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo kwenye ukurasa 5.