Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 3/22 uku. 32
  • Siku Iliyobadili Maisha Yake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siku Iliyobadili Maisha Yake
  • Amkeni!—1995
Amkeni!—1995
g95 3/22 uku. 32

Siku Iliyobadili Maisha Yake

MWANAMKE mmoja mchanga kutoka Arizona, Marekani, alisema kuwa alikuwa amekuwa mwenda-kanisani lakini akaja kutamaushwa na dini. Hatimaye alimweleza Mungu hivi katika sala: “Siendi kwenye makanisa yoyote mengine. Nitaishi maisha yangu katika njia nijuayo kuwa sawa, na nitajaribu kuwa mtu mwema.”

Mwanamke huyo alielezea kilichotukia baadaye: “Shangazi yangu alinipigia simu na kusema kwamba angekuwa sehemu za kwetu kuhudhuria siku ya kusanyiko la pekee la Mashahidi wa Yehova. Aliomba ikiwa yeye na binamu yangu wangeweza kulala kwenye nyumba yangu. Na akauliza: ‘Ungependa kwenda nasi?’ Nakumbuka jibu langu: ‘Kwa nini isiwe hivyo? Sina lolote muhimu la kufanya.’ Upendezi wangu katika dini ulikuwa waelekea kufa.

“Nyakati zote nilielezwa nitahadhari dhidi ya Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo wakati wa kusanyiko, nakumbuka nikiwa mwangalifu sana. Hata hivyo, hakukuwa na fumbo kuhusu lililosemwa juu ya kusudi la awali la Mungu la kuwa na dunia paradiso na kusudi la Mungu halikuwa limebadilika. Niliketi pale na hisi hii changamfu nikitazama familia zikiketi pamoja na kuonyesha roho ya umoja. Niliinamisha kichwa changu na kwa kimya kumwomba Mungu hivi: ‘Hii ni kweli? Hili ndilo nimekuwa nikitafuta?’

“Nilipoondoka siku hiyo, nilitazama watu wakikumbatiana na kubusiana kwaheri wakiwa na nyuso zenye tabasamu nyangavu. Ningeweza kuona katika nyuso zao kwamba hakukuwa na shaka lolote katika akili au mioyo yao juu ya itikadi yao na juu ya ni nani Yehova na lile ambalo amewafanyia. Tangu siku hiyo na kuendelea, nilianza kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova na sijaacha tangu wakati huo. Siku ya kusanyiko la pekee iliyofuata, katika 1988, nilifananisha wakfu wangu kwa Yehova hadharani kwa ubatizo wa maji na kuwa sehemu ya familia hiyo yenye kupendeza.”

Ikiwa ungependa kujifunza mengi kuhusu itikadi na utendaji wa Mashahidi wa Yehova, tafadhali wasiliana nao kwenye Jumba la Ufalme, au uandike ukitumia anwani ya karibu nawe iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Hisi changamfu ya familia huenea katika vikusanyiko vikubwa vya Mashahidi wa Yehova, kama inavyoonekana hapa katika Urusi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki