Mwalimu Alikifurahia
“Mwaka uliopita katika kozi yangu ya Kiingereza ya kidato cha pili, tulitumia siku kadhaa kujifunza tofauti kubwa ya dini katika ulimwengu,” akaandika kijana fulani kutoka Michigan, Marekani. Huyo mvulana alileta shuleni nakala ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Yeye alieleza hivi:
“Nilifikiria hasa mwalimu wangu angekiona kikiwa chenye kupendeza kwake. Nilifurahi kumwona akisoma hicho kitabu wanafunzi walipokuwa wakifanya kazi ya shule. Ingawa hivyo, waweza kuwazia jinsi nilivyoshangaa wakati, kabla ya saa za somo hilo kwisha, mwalimu alikatiza wanafunzi kutoka walichokuwa wakifanya na kutusomea sura yote ya kwanza kwa sauti. Hata alituelekeza tuandike mambo ya muhimu kuihusu.
“Siku chache baadaye, alitumia hicho kitabu tena katika maagizo ya darasani, akiwapa wanafunzi mgawo wa kuandika ripoti nyingine, akiwaambia wangeweza kutumia kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kikiwa msingi. Hicho kitabu kilitumiwa kwa muda wa saa nzima.”
Ikiwa ungependa nakala ya Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu au kupenda funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo kwenye ukurasa 5.